Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein Ameongoza Kikao cha Kamati Maalum ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar.
Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Afisi Kuu ya CCM ,Kisiwandui Zanzibar.
Pamoja na mambo mengine Kikao hicho kimepokea na kujadili Taarifa ya mapendekezo ya Wana CCM walioomba kuteuliwa Kugombea Nafasi ya Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi, kutoka katika Majimbo na Nafasi ya Uwakilishi Viti Maalum vya Wanawake katika Mikoa ya Zanzibar.
Kikao hicho ni Maalum kwa mujibu wa matakwa ya Katiba ya Chama cha Mapinduzi ya Mwaka 1977.
Aidha Chama cha Mapinduzi kinaeleza kuwa Kikao hicho ni Miongoni mwa Vikao vyake vya Uongozi vya Kitaifa vinavyofanyika kwa mujibu wa kanuni na miongozo ya CCM.